‘Hadithi ya kale, inayoishi’
HUSSEIN O. MOLITO
0718 97 56 59/ 0765 68 4870
Aliangaza macho yake mlangoni ili kutazama kama kuna mtu anachungulia. Alipohakikisha kuna usalama wa kutosha, akauchukua mkono wa Mtafiti Gibson na kuanza kutafuta mshipa wa damu ili aweze kuipitisha sumu hiyo haraka kwenye mfumo wa damu.
Aliachia tabasabu baada ya kuupata, sasa alianza kulengesha sindano hiyo. Akachoma taratibu na kuhakikisha imefika mpaka mwisho.
“Kwa heri rafiki.” Dokta Gibsoni akaongea hayo na kuachia tabasamu.
Kabla hajabonyeza kitufe cha sindano hiyo ili kuruhusu bomba la sindano kupitisha sumu hiyo na kuingia kwenye mishipa ya damu, alishtushwa na sauti ikikohoa nyuma yake; alikua Dokta Kelvin.
“Dunia ni kubwa kuliko sisi... Hupaswi kufanya yote hayo kwa kushindana na dunia.” Dokta Kelvin aliongea hayo na kumfanya Dokta Miley aichomoe haraka sindano hiyo na kuitupia pembeni. Maana kichupa kilichuka kwenye kitoroli kidogo kiliweza kuonesha nembo ya sumu anayoitumia kwenye bomba hilo la sindano.
“kwa hiyo ulikua unanichunnguza?” Dokta Miley akauliza.
“hapana, nilisahau jambo muhimu sana, kumuachia nesi maagizo juu ya uangalizi unaotakikana kwa wagonjwa ambao wanaonekana wana ufahamu kwa macho, ila kiukweli hawana ufahamu. Ndo ikawa bahati kwake.” Dokta Kelvin akaongea hayo na kumfanya Dokta Miley amsogelee.
“mimi na wewe hatujaonana siku ya leo, hiki kilichotokea hujakishuhudia. Nitafurahi ukiacha kila ulichokiona kuwa siri yako.” Dokta Miley akaongea hayo na kuondoka kwenye chumba hicho bila kusubiri majibu yoyote kutoka kwa daktari mwenzake.
**********
Mlengaji alishahakikisha kwa kile alicholenga, akaachia risasi mbili haraka haraka zilizokwenda kwa spidi sana.
‘paaah, paah’
Milio ya kushtusha ilisika kwa sauti ndogo, ila urukaji wa damu iliyochafua shati la Mohammed, uliweza kuwafanya wapatwe na mshtuko.
Muanguko wa binti aliyepigwa risasi uliweza kuwajulisha baadhi ya watu waliokua hapo kwamba sehemu hiyo si salama.
Mlengaji akarudi garini haraka na kumuamuru dereva aondoe gari kwa kasi.
Kila mtu aljificha ili ajaribu kuokoa nafsi yake. Mohammed na binti yake Raniya walikua wamekumbatiana huku wakiwa hawaamini kilichotokea.
Simu ikaita kwenye gari alilokuwemo mlengaji.
“naam bosi.” mlengaji akaongea baada tu ya kupokea simu.
“bila shaka una habari njema za kunipa muda huu.” mkuu wa kitengo akauongea.
Mlengaji akatafakari kidogo, kisha akaongea.
“nilimuweka kabisa kwenye malengo, hata sijui kitu gani kimetokea. Nikajikuta nimempiga risasi mtu asiyehusika.” mlengaji akaongea hayo na kumfanya mkuu wa kitengo kupandwa na ghadhabu.
“unaniambia upuuzi gani? Kipi kilichokufanya umlenge mtu mwengine ilihali wewe ni hodari wa kazi yako?”
“wakati nalenga, huyo msichana hakuwepo... Ila baada ya kuachia risasi akawa amesimama mbele yake. Nikawa nimempiga yeye risasi zote mbili.” mlengaji akatoa ushuhuda.
“huyo msichana atakua hai kweli?” mkuu wa kitengo akauliza huku safari hii akiwa ameipooza sauti yake.
“sidhani kama atapona... Maana risasi zote zimepiga mgongoni.” Majibu hayo yakazidi kumnyong’onyesha.
“lakini una uhakika hakuna mtu aliyewaona?”
“ndio mkuu.”
Baada ya majibu hayo. Mtu aliyewapa kazi ya kumuua Samira akakata simu.
Watu walikua wamemzunguka binti aliyepigwa risasi na kuanguka chini. Kwakua alikua amedondokea kifudifudi, hakuna aliweza kuiona sura yake. Ila askari walipofika na kuugeuza mwili wa binti huyo, Samira alipigwa na butwaa baada ya kumuona binti yuleyule anayetangazwa kuleta madhara kila leo.
Alikua ananifuatilia, au nilitakiwa kuuwawa ndo ameniokoa? Samira alijiuliza swali hilo wakati walipokua kwenye kumbatio la baba yao aliyewasihi wabaki chini ya meza kwa usalama wao.
“baba, huyo binti aliyepigwa risasi. Ndo huyo aliyeniweka kisangani hadi nikaitwa polisi.” Samira alimuelezea baba yake, hapo ndipo naye akamtazama binti huyo kwa umakini.
Askari walikuja kuwatoa hapo walipo na kuwaambia kua wamezunguka maeneo yote na mahala hapo ni salama kwa muda huo. Waliwauliza kama kuna mtu amejeruhiwa baada ya nguo zao kuonekana kurukiwa na damu za binti huyo.
“Kwani amekufa?” Samira akauliza baada ya kuona wanamuingiza kwenye kwenye gari yao.
“hatujui, ndo tunamuwisha hospitali. Kwani unawafahamu ndugu zake?” Askari akauliza.
“Hapana, ila sura ya huyo binti si ngeni kwangu. Ningependa kujua anapelekwa hospitali gani.” Samira akauliza.
“Muhimbili.” Askari akajibu.
“tunawaze kuwafuatilia, nahitaji kujua maendeleao yake.... Hata kama kafa, nahitaji kujua pia.” Samira akaongea hayo na kumuangalia baba yake ambaye alikua anamminya kama ishara ya kumkataza kutojihusisha na maswala hayo.
“haina shida, tunaweza kuongozana.” Askari akajibu hivyo na kwenda kwenye gari iliyopandishwa mwili wa binti huyo, na yeye akaongozana na ndugu zake hadi kwenye gari yao.
“iwe kwa heri au ubaya, sijapenda kabisa maamuzi yako ya kushadadia watu. tena hawa askari, hawana muamana kabisa hasa kwa kesi kama hizi za mauaji. Wanaweza hata kusema wewe ndo shuhuda na uwasaidie kwenye upelelezi.” Mohammed alifoka walipokua njiani wakiifuatilia gari ya polisi.
“kuna uwezekano mkubwa zile risasi nilitakiwa kupigwa mimi... Maana usawa aliodondokea binti yule ni wangu kabisa. Kwanini tusihakikishe usalama wake? Na kama kafa kwanini tusiombe kuzika, maana nafahamu kama akili zake sio nzuri na hana ndugu wa kumfaa hata kwa nguo.” Samira aliongea maneno hayo na kumfanya baba yake awe mpole.
**********
Inspekta Salim akiwa hosptali, alifuata taratibu za awali na kumpeleka salehe kumuona daktari. Yeye alirudi kukaa benchi ili aweze kusubiri majibu ya vipimo atakavyopimwa mgonjwa wake.
Akiwa hapo, simu yake ikaita na jina la Samira ilikajitokeza.
“habari Samira, kwema?” Inspekta Salim alipokea simu hiyo huku akiwa na hofu, maana siku hiyo alihisi kujawa na mkosi.
“Mimi ni mzima kabisa. Ila kuna tukio limetoka Triple Seven muda mchache uliopita, yule kiumbe unayemtafuta; amepigwa risasi na watu wasiojulikana.” Samira akatanabaisha. Mapokeo ya mshangao yakazidi kwa Inspekta Salim.
“Amekufa?” akauliza kwa hamaki.
“kiukweli sijui, ndo tunamfuatilia hapa. Amechukuliwa na polisi anapelekwa Muhimbili muda huu.” Samira akamalizia kuelezea habari hiyo.
“mimi pia nipo hospitali, kuna kijana amevamiwa na watu haohao wasiojulikana. Ngoja nimalizane naye kisha nitawasiliana na wewe ili nijue mambo yanaendaje huko. Kwa lolote litakalotokea, usisite kuwasiliana na mimi.” Inspekta Salim akasisitiza.
“Sawa.” Samira akajibu na kukata simu. Akarejesha simu yake mkobani.
“hivi hakukutajia jina lake?” Mohammed akauliza baada ya kuona binti yake ameshamaliza kutoa taarifa kwa askari.
“sikumbuki chochote... Ila akifa roho itaniuma sana.” Samira akajibu na kumfanya Rabia amuangalie kwa jicho pembe.
“Usituchekeshe wakati tumetoka kunusika kufa... Yaani huyo binti anavyosababisha madhila kwa binaadamu bado unamuonea huruma? Na hao polisi hawajamjua tu, wangemmalizia kabisa kwa kumpiga risasi zingine.” Rabia akaongea, hata baba yake alimtazama.
“binti yangu, umeipata wapi roho ya kikatili kama hiyo?” Mohammed aliuliza na kumfanya Rabia aone aibu na kutazama chini.
Mwendo wa kuifuata barabara ukfikia kwenye kona, na baadae kwenye mzunguko na kuwajulisha kuwa wameshafika kwenye geti la kuingilia hospitali ya Muhimbili. Walichukua kadi ndogo kwa mlinzi na kuifuata gari ya polisi hadi sehemu ya wodi ya wagonjwa mahututi. Binti huyo akapokelewa, lilipohitajika jina moja kwa mtu aliye karibu naye, Samira alikubali liandikwe jina lake.
Watu wa huduma ya kwanza waliwahi na kitanda. Haraka akawahishwa wodini katika harakati za kuyapigania maisha yake.
Haya... Kiumbe wa ajabu yamemkuta. Alikua akijaribu kuokoa maisha ya Samira au na yeye alikua na dhamira nyingine? Endelea kufuatilia.
Ukumbuke tu....... Hii ni Typhin, Hadithi ya kale inayoishi...








0 comments:
Post a Comment
comment