Friday, January 10, 2020
DEREVA TOYO 09
Dereva toyo Mtunzi:Richard Yassin Sehemu ya 9 Wasiojua maana ya usiri katika mioyo yao.Kwangu mimi niliandika historia kwani sikuwahi kupinduka na mama wa makamo na kumgalagaza.Hivyo kutokana na njaa niliamua kwenda kupata chakula cha kutuliza minyoo iliyokuwa ikinisumbua katika tumbo langu na nilipomaliza kula niliona ni vyema nirudi kupumzika.Nilingia ndani na kuweka muziki laini uliokuwa ukinibembeleza ila safari hii niliishia kulala na kutokana na uchovu nilijikuta kumepambazuka na sikuwa nimeweka neti.Asubuhi niliamka kama ilivyo ada nikanyoosha nguo zangu zilizokaa mkao mzuri wa kung'aa ili niweze kwenda kutunukiwa zawadi yangu.Nilivaa shati jeupe na suruali ya bluu huku nikitundika koti la bluu na tai ya bluu.Kwa namna nilivyovaa mtu wa kawaida angehisi kuwa ninafanya kazi ya uanasheria mjini.Hivyo nilipomaliza kuvaa moja kwa moja nilikwenda kuchukua uba ili inikimbize hadi maeneo ya Mlimani city mahala ambapo palifanyika makabidhiano ya pesa hizo katika moja wapo ya matawi ya benki ya Nmb.Siyo siri siku hiyo niliitendea heshima ya suti kwani waswahili husema unapovaa suti hairuhusiwi: 1. Kutembea kwa miguu masafa marefu. 2.Kula kwa kutumia kiganja. 3.Kujifuta jasho kwa mkono 4.Kula barabarani na mengine mengi. Hivyo mara tu nilipotoka nje ma Abasi alinotupia maneno yake ya kusifu maneno ambayo yaliukosha moyo wangu ingawa nilikuwa sina hela mfukoni kwangu kwani kwa sifa zile nilizopewa ningemtuza.Hivyo kutokana na kuwa na usafiri binafsi nilifika eneo la Mlimani City ndani ya muda mfupi.Na nilipofika nilionyesha kitambulisho changu ili watambue jina langu na hivyo walipoliona jina l hilo,nilikaribishwa na kukaa viti maalumu ili kusubiria uongozi mzima uje kuwakabidhi watu pesa zao walizojishindia.Nachoshukuru sikuwa peke yangu kwani palikuwa na watu wengine wawili waliojitwalia pesa hizo pia ingawa viwango vilikuwa tofauti na kila mmoja ilikuwa ni siri yake kwani....Itaendelea!!!
PAKUA APP YETU
Kwa wale wapenzi wa Mziki Mzuri,filamu nzuri na Hadithi nzuri kutoka kwa waandishi mbalimbali, blog yetu ya Burudani, Tunapenda Kuwataarifu kuwa:
> Kama Hautumii App Basi tunakuomba PAKUA APP YETU MPYA HAPA Ili uweze Kupakua Nyimbo Mpya kirahisi
> Pia Utapata Taarifa kila wimbo Mpya unapotufikia.
PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file
Official android App for www.cleverwebtz.blogspot.com
This application is developed with the following key features:
• Listening Music online with latest collection of tracks
• Download Music for listening offline
• Read story from different author
•watch movies online and download
• Listen to Music and do other things with a convenient way with playing background modes, customizable through the Notification bar (notification).
PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file








0 comments:
Post a Comment
comment