Friday, January 17, 2020
TYPHIN 09
‘Hadithi ya kale, inayoishi’
HUSSEIN O. MOLITO
0718 97 56 59/ 0765 68 4870
“sasa unasubiri nini kufanya kazi yako kama nafasi ipo?… muulie mbali.” Sauti ya mamlaka ikasikika upande wa pili, simu ikakatwa.
Taratibu kijana huyo alifungua begi lake na kutoa bunduki yenye uwezo wa kupiga masafa mrefu. Akafunga kiwambo cha sauti ili aweze kufanya tukio lake bila watu wengine kushtushwa na sauti ya risasi pindi atakapoifyatua.
Alihakikisha kama kuna risasi za kutosha, baadha ya kuridhika akaanza kuchungulia kwenye kifaa alichokifunga juu ya bastola hilo. Aliweza kumuweka Samira katika usawa mzuri. Alipandisha mshale wa malengo kwenye kifua cha binti huyo.
Samira akiwa anacheka, hakujua kua sekunde chache kutoka hapo hatokua hai endapo tu mlengaji atafyatua risasi kadhaa kifuani kwake.
Familia ilionekana kuwa na furaha sana kwa kutaniana na Samira hiki na kile. Mlengaji naye taratibu akapeleka kidole kwenye kifyatulio cha rasasi.
***********
Giza likiwa limetanda, hatua zikasikika zikisogea upande uliokua na mwanga wa taa. Akiwa peku, aliweza kufika eneo hilo lililokua na watu wawili wakipita na mmoja akifanya biashara. Alijisogeza hadi hapo kwenye biashara ya chipsi. Palikua na utulivu mkubwa kwakua hakukua na mtu mwingine zaidi ya muuzaji ambaye alikua anageuza chipsi zingine zilizokua jikoni. Alifika na kusimama hapo kwa muda bila kuongea kitu chochote, macho pima kwenye kabati lililosheheni vitu mbalimbali vya kutamanisha.
Muuza Chipsi alimshangaa binti huyo ambaye alisimama mbele ya kabati la chipsi bila kuongea kitu chochote.
“karibu dada, chipsi za moto zinatoka jikoni sasa hivi.” Muuza chipsi aliongea baada ya kuhisi huyo binti huenda ni mteja wake.
Hakujibiwa, zaidi binti huyo alikua akiwatumbulia macho samaki wakavu waliosimamishwa vizuri kwenye kabati hilo la chipsi.
“unahitaji samaki?” Muuza chipsi akauliza baada ya kutoka na kumsogelea binti huyo. Swali hilo likajibiwa kwa kichwa. Maana ni kweli alikua akihitaji.
“hawa wakubwa elfu tano na hawa wadogo elfu m bili mia tano.” muuza chipsi akanadi bei zake.
Binti huyo akaonesha samaki mkubwa aliyemvutia. Muuza chipsi akaenda kumchukua samaki hiyo na kumuweka kwenye mfumo.
“nikufungie pilipili?” muuza Chipsi akauliza, hakujibiwa.
Haikumshangaza sana, maana wasichana wengi wa mtaa huo walikua wakijisikia kutokana na maisha mazuri waliyoyakuta. Waliona hana hadhi ya kuwaongelesha zaidi ya kuwauzia wanachohitaji na yeye kupewa ujira wake.
Aliamua kumfungia binti huyo na kumletea. Alistaajabu baada ya kuona akifungua mfuko hapohapo na kuanza kumla bila kutoa miba. Baada ya kumaliza, alimuonesha samaki mwengine.
“hela ipo wapi kwanza.” muuza chipsi akauliza baada ya kumtazama binti huyo miguuni. Miguu ilikua imejaa vumbi; yupo peku, mwendo wa kumsaidia bata.
Kama mtu asiyeelewa lugha, binti huyo bado akakazania akaonesha samaki anayemuhitaji.
“we binti, utaenda kulala kwangu kama ukileta mchezo na pesa. Leta kwanza elfu kumi ndo nikupe samaki mwengine.” muuza chipsi akapandisha sauti.
Kwa kawaida binti huyo hua hapendi kelele, hasira zikaanza kumpanda kiasi cha kumuangalia muuza chipsi kwa macho makali.
Alipiga ngumi nzito kwenye kioo kilichopo mbele yake, kikavunjika. Akawatoa samaki wawili na kuanza kuwala kwa pupa huku akihema kwa kufoka kwa sauti ya kuogofya.
Muuza chipsi alishika kichwa kwa kile alichokiona muda huo. Wakati akiwa amepigwa na bumbuwazi asijue afanye nini kwa wakati huo, alimshuhudia binti huyo akifukutwa na kitu mfano wa moto kwenye koo lake. Hofu ya kuhisi binti huyo si binaadamu wa kawaida, ikamtanda.
Alipojaribu kukimbia, alipigwa ngwara na kuanguka kama gunia la viazi. Sasa mikono ikiwa juu akimuomba binti huyo asimdhuru. Maana tayari alishamfikia na kumzuia kwa kumkalia juu yake, uso wa binti alibadilika na kuwa wakutisha. Macho na shingo vilizidi kumtisha muuza chipsi kwa mngao wake mfano wa muwako wa moto.
************
“eeh Darling, upo wapi?”
“nipo njiani, naelekea kununua chipsi kwa Salehe.”
“Jamani, ujue Darling Chipsi si nzuri eeh, usiziendekeze sana.”
“Najua mume wangu, ila leo nimechoka sana. Acha tu nikanunue, kesho nitapika.”
“sikia, we rudi. Mimi naenda kununua samaki hapo kwa Salehe, mchele si upo?”
“ndio Darling.”
“basi we tulizana, miye mwenyewe nitaingia jikoni. See you soon.”
“ok, take care Darling.”
Hayo yalikua maongezi ya wapendanao. Inspekta Salim alikua njiani akielekea kwa mchumba wake. Hakujua kua wakati huo, Salehe muuza chipsi alikua katika hatua ngumu za kutetea maisha yake.
Baada ya kukata simu, alikanyaga mafuta ili kuwahi kwa Salehe. Alipaki gari yake na kushuka. Mshangao ukampata baada ya kuona mparakanyiko wa chipsi na vioo vilivyotapakaa kila mahali, alihisi kuna tatizo.
Akachomoa bastola yake ndogo aliyopenda kuiweka kwenye mfuko wa kote na kuanza kuangaza macho yake huku na huko.
Eneo hilo lilikua kimya sana. Na hiyo ni kutokana na kupooza kwa mtaa huo. Giza linapoingia, ndo kabisaa. Isingekua wateja kadhaa ambao hupata huduma mida ya usiku hasa hapo kwa Salehe, basi ungemshauri asifanye biashara usiku kwa usalama wake binafsi.
Inspekta Salehe aliita jina la muuza chipsi bila ya mafanikio. Aliingia kwenye fremu yake na kuangaza maeneo ya karibu, hakumuona pia.
“Haloo Darling, nahisi Salehe amevamiwa na watu wabaya. Acha nifuatilie. Nitakuja na chipsi tu. Ila uvumilie hata kama nikichelewa.” Inspekta Salim akapiga simu kwa mchumba wake na kumpa taarifa. Wakati akiwa makini huku bastola yake ameiweka vizuri, aliweza kusikia sauti kwa mbali ya mtu akihema. Aliwahi mtaroni ambapo ndipo sauti hiyo inapotoka, aliweza kumuona Salehe na kumsaidia kutoka.
Alikua anaweweseka huku moyo ukimdunda kupita kiasi.
“Tulia, upo kwenye mikono salama.” Inspekta Salim alimtuliza Salehe. Akamkokota hadi kwenye fremu yake ya biashara.
Hakutaka kumuuliza chochote kwa wakati huo zaidi ya kuanza kumkagua. Baada ya kuhakikisha amepumzika kwa muda wa dakika kumi, ndipo alipoanza kumuhoji.
“umeumia sana?” Inspekta salim aliuliza baada ya kutoona majera nje ya mwili wake.
“hapana.” Salehe akajibu.
“unaweza kunieleza ni kipi kilichokukumba?” Inspekta akauliza. Salehe akatingisha kichwa, akikanusha kuelezea.
Inspekta alitambua hali aliyokua nayo Salehe kwa muda huo.
“Tulia, acha nikusaidie kuweka vitu ndani. Tufunge na tuelekee hospitali.” Inspekta Salim akaongea hayo na kwenda nje. Akaanza kuingiza vitu ndani mpaka alipomaliza.
Baada ya kufunga, aliongozana na Salehe hadi kwenye gari yake. Akatekenya funguo na safari ya kuelekea hospitali ikaanzia hapo.
“nimefanikiwa kumpata, ndo tunaelekea hospitali muda huu.” Inspekta Salim alimpasha habari mchumba wake.
“Mungu mkubwa, kaumia sana?”
“Hana majeraha kwa nje… ila kwa hali yake, nahisi kaumia ndani kwa ndani. Ndo maana nampeleka hospitali kwa uchunguzi zaidi.”
“sawa, utanijuza basi hali inavyoendelea.” mpenzi wa Inspekta Salim akaongea hayo na kukata simu.
**********
Baada ya kupatikana kwa utulivu wa hali ya juu, Dokta Miley alimuangalia Mtafiti Gibson kwa macho ya hasira.
“Natamani ungekua na kumbukumbu zako ili uweze kuniona kwanza muuaji wako siku ya leo. Ulikua unatamba sana kwa tafiti zako na ukatufanya sisi tunaokesha kufanya vitu bora zaidi yako tuonekane si lolote si chochote. Sasa leo ndo mwisho wako, na jina la Dokta Miley linaenda kufuta kumbukumbu zako zote. Ulikua rafiki hapo awali kabla hatujamaliza chuo, ila kwa sasa umekua adui wa jina langu. Ulale salama Gibson.”
Dokta Miley akachukua Sindano iliyokua kwenye mkoba wake na kichupa kidogo kilichokua na sumu ndani yake. Akavuta sumu hiyo iliyokua kwenye kichupa kwenye sindano tupu na kuhakikisha imejaa mpaka mwisho.
Aliangaza macho yake mlangoni ili kutazama kama kuna mtu anachungulia. Alipohakikisha kuna usalama wa kutosha, akauchukua mkono wa Mtafiti Gibson na kuanza kutafuta mshipa wa damu ili aweze kuipitisha sumu hiyo haraka kwenye mfumo wa damu.
Aliachia tabasabu baada ya kuupata, sasa alianza kulengesha sindano hiyo. Akachoma taratibu na kuhakikisha imefika mpaka mwisho.
“Kwa heri rafiki.” Dokta Gibsoni akaongea hayo na kuachia tabasamu.
Inaweza kuwa majonzi kwenye sehemu inayofuata. Tukutane tena Jumatano.
Kumbuka tu, hii ni TYPHIN, Hadithi ya kale inayoishi…
Kama umeipenda… like, comment kisha share na wenzako wapate kuifuatilia. Uwe na usiku mwema.
PAKUA APP YETU
Kwa wale wapenzi wa Mziki Mzuri,filamu nzuri na Hadithi nzuri kutoka kwa waandishi mbalimbali, blog yetu ya Burudani, Tunapenda Kuwataarifu kuwa:
> Kama Hautumii App Basi tunakuomba PAKUA APP YETU MPYA HAPA Ili uweze Kupakua Nyimbo Mpya kirahisi
> Pia Utapata Taarifa kila wimbo Mpya unapotufikia.
PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file
Official android App for www.cleverwebtz.blogspot.com
This application is developed with the following key features:
• Listening Music online with latest collection of tracks
• Download Music for listening offline
• Read story from different author
•watch movies online and download
• Listen to Music and do other things with a convenient way with playing background modes, customizable through the Notification bar (notification).
PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file








0 comments:
Post a Comment
comment