CLEVER WEB TZ

Breaking News
Loading…

Pages

TANGAZA NASI

TANGAZA NASI
ENEZA BIASHARA YAKO

Friday, January 10, 2020

TYPHIN 06


TYPHIN 06
‘Hadithi ya kale, inayoishi’
HUSSEIN O. MOLITO
0718 97 56 59/ 0765 68 4870
La haaulaaa!
Binti kapotea machoni mwake kwa kasi ya ajabu. Mbali na ujasiri mkubwa aliokuanao Inspekta Salim, kile kijasho chembamba cha woga kikaanza kumtiririka kwa kasi huku akikosa uamuzi wa kubaki kwenye gari ama kushuka ili amfuatilie binti huyo ni wapi alipoenda.
Akili ya ukombozi ikamwambia Inspekta Salim awashe gari yake na kuondoka eneo hilo haraka sana.
Kitete kikamfanya azime gari badala ya kuiruhusu iondoke. Akajikuta anahema mfano wa mtu aliyetoka kuogelea maji ya kina kirefu kushinda uwezo wake.
akazungusha funguo ya gari, safari hii gari nayo ikagoma kuwaka, akachachawa.
“waka baba, tutakufa hapa. Waka basi.” Akajikuta akilibembeleza gari huku akijaribu kuzungusha funguo mara kadhaa.
“Mbona betri bado jipya jamani… mbona linagoma kupiga stata?” akajiuliza mwenyewe huku akijaribu kuomba msaada kutoka kwa vitu visivyo na uhai. Uoga nao ukizidi kuutafuna moyo wake, harufu ya kifo alihisi inazidi kutanda ndani ya gari yake.
Alipojaribu kuiwasha gari hiyo kwa mara nyingine, safari hii ikakubali kuwaka.
Huo mwendo wake sasa, almanusura apate ajali kwa kuliingiza gari lake mtaroni kwa jinsi alivyokanyaga mafuta kwa nguvu.
Aliendesha gari yake kwa mfumo wa alijojo huku moyo wake ukidunda hobelahobela kwa hofu kuu aliyokuwa nayo wakati huo.
Alimshukuru Mungu na Malaika wake kwa kuweza kumfikisha salama usalimini nyumbani kwake na kuegesha gari nje ya geti. Alichokumbuka ni kuizima na kutoa funguo. Baada ya kufungua geti la nyumbani kwake, hakutamani kulirudia tena gari lake nje ili aliegeshe kwa usalama, aliona ni heri wezi wakaiba gari kuliko kutoka nje na kukutana tena na kiumbe huyo wa ajabu.
Aliingia ndani kwake na kujifungia, jasho lilitota kwenye nguo zake huku akihisi baridi mwilini mwake.
Aliliendea jokofu lake na kutoa kikontena kidogo kilichokua na mabarafu madogo madogo. Akachukua mzinga wa Joni Mtembezi na kuijaza kwenye bilauri iliyojaa barafu ndogo ndogo na kuanza kunywa kinywaji hicho kwa pupa.
“Hivi ni nimeonana na jini ama nipo kwenye ndoto?”
Inspekta Salim alijiuliza baada ya taswira ya binti huyo kujirudia kwenye ubongo wake. Kinywaji kiliendelea kushuka kwa fujo kwenye koo lake, lakini hakikuweza kumpa matokeao anayoyataka. Kimea kiligoma kabisa kuupumbaza ubongo wake.
Akajikusanya pale alipo na kwenda kujitupa kitandani kwake kama mzigo wa viazi. Akiwa hapo, alilazamisha usingizi, na baada ya muda ukakubali.
Alishtushwa na mlio wa simu yake, aliamka huku akiwa na wenge na kuangalia nani apigaye. Alipatwa na mshtuko mkubwa, akaipokea simu hiyo haraka.
“Mkuu!”
“hivi umesahau kama tuna miadi ya kukutana leo hii?”
“Nakuja mkuu, sasa hivi.”
Inspekta Salim akaongea maneno hayo, simu ikakatwa. Aliangalia saa yake ya ukutani, ilimsomea kuwa muda huo ni saa nne na nusu. Akajikusanya haraka hapo kitandani na kuelekea bafuni. Huko aliuchukua mswaki wake haraka na kuupeleka mdomoni bila kuweka dawa. Alifungulia maji kwenye bomba la mvua na kuanza kuoga huku akiendela kuswaki. Alifanya hayo yote ilimradi aweze kukimbizana na muda ambao mpaka wakati huo ulimshamtangulia.
Alitumia dakika kumi kujiandaa na kutoka. Akingia kwenye gari yake na kuelekea ofisini kwa mkuu wake wa idara.
Foleni nayo haikua rafiki mzuri kwake, aliishia kutukana madereva wenzake barabarani na kuna wakati alitamani hata kupanda juu ya magari mengine ilimradi awahi kufika ofisini kwa bosi wake.
Mpaka anaifika Posta, tayari ilishatimia saa tano na nusu. Alilaani kila kilichomchelewesha na kupiga hatua ndefu ndefu kuelekea kwenye lifti ili aweze kufika ghorofa ya saba.
Watumiaji nao wakawa wengi, hivyo lifti ikachelewa kushuka chini kwa dakika nne zaidi. Mpaka hapo, alikubali kuwa mpole. Ilipofika akaingia huku kichwa chake kikiwa na mawazo tele.
Baada ya kufika ghorofa ya saba, alisogea mapokezi na kuomba kuonana na mkuu wake. Akaruhusiwa baada ya dada wa mapokezi kufanya mawasiliano na kumtajia bosi wake ujio wa Inspekta Salim pale.
“Samahani Mkuu..” Inspekta Salim aliongea hayo alipofungua mlango, akaikatisha kauli yake baada ya kukuta kuna idadi ya watu wapatao wanne humo ndani.
“Karibu Inspekta Salim, tulikua tunakusubiri wewe tu hapa ili tuanze hiki kikao cha dharula.” Mkuu wa idara aliongea hayo na kumfanya Inspekta Salim aende kukaa kwenye moja ya viti vilivyopangwa vyema ofisini humo.
“Inspekta Salim, una haki ya kushangaa wingi wa watu tofauti na mategemeo ya miadi yetu. Ila kuna jambo limetokea na imetupasa tukutane kwakua wewe ndo unashikilia faili la kesi hiyo. Kuna binti analeta shida huko mitaani, umefikia wapi kwanza kwenye kutimiza majukumu yako juu ya hili jambo?”
Inspekta Salim alisisimkwa mwili baada ya kutajiwa habari za binti huyo.
“nalifanyia kazi mkuu, nipo kwenye hatua za mwishoni za kumtia nguvuni.” Inspekta Salim akajibu na kuwaangalia watu waliokua humo ndani kwa zamu.
“Inspekta Salim, hili jambo linaweza kukushushia heshima yako kama ukilichekea, hivi unafahamu hawa wanaokutazama ni kina nani?” swali hilo likamfanya Inspekta Salim awatazame tena watu hao ambao ni wageni machoni mwake.
“Hapana, bado sijawajua mkuu.” Inspekta Salim akajibu baada ya kujiridhisha kutowafahamu.
“Hawa ni wageni kutoka Rwanda, huyu ni Waziri wa mambo ya nje na hii ni familia yake. Leo hii asubuhi wameshambuliwa na huyo msichana na mtoto wao hivi sasa yupo hospitali. Sasa nakupa oda, baada ya masaa sabini na mbili, nataka nipate taarifa za kukamatwa kwa msichana huyo. Kama ni kichaa basi daktari athibitishe akiwa chini ya uangalizi wetu.” Mkuu wa kitengo akaongea maneno hayo na kumuangalia Inspekta Salim kwa macho makali.
“Sawa mkuu.”
ilikua ni Amri, hivyo kukubali ilikua ni lazima kwake. Akaruhusiwa aendelee na majukumu yake.
japokua alikubali kuifanya kazi hiyo, ila moyo wake ulitamani kusema jambo kwa mkuu wake juu ya kiumbe huyo ambaye ameyashuhudia kwa macho yake mauzauza aliyokuwa nayo.
baada ya kushoka kutoka kweli lifti, akaliendea gari lake taratibu tayari kwa kurudi kituoni ili aweze kupanga mikakati ya kumnasa kiumbe huyo.
“Kwanini anazuru watu?”
Inspekta Salim alijiuliza swali baada ya kufika kwenye foleni eneo la mataa.
Akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa, kioo kidogo kilichopo ndani ya gari yake, kilimuonesha kitu kilichomfanya ageuke nyuma haraka.
Hamadi!
uso wake ukakutana na sura ya binti huyo akiwa siti ya nyuma ya gari yake.
“Nataka maji.”
kwa mara ya kwanza aliweza kuisikia sauti ya binti huyo mwenye macho makali ikimuamrisha. Akajikuta akikubali kwa kichwa huku sauti ikigoma kutoka. Akashtushwa na sauti za honi kutoka nyuma yake, maana muda huo taa zilisharuhusu na alikua amebung’aa tu baada ya kumuona binti huyo mwenye maajabu akiwa ndani ya gari yake.
Hakujua alipanda wakati gani, na amemfuata akiwa na nia gani baada ya kumfanyia vitimbi usiku wa siku iliyopita.
Haya, waiteni ndugu zenu waje kwa wingi ili tuweze kuendelea…
Kumbuka tu, hii ni TYPHIN, Hadithi ya kale inayoishi………..

0 comments:

Post a Comment

comment

PAKUA APP YETU

Kwa wale wapenzi wa Mziki Mzuri,filamu nzuri na Hadithi nzuri kutoka kwa waandishi mbalimbali, blog yetu ya Burudani, Tunapenda Kuwataarifu kuwa:

> Kama Hautumii App Basi tunakuomba PAKUA APP YETU MPYA HAPA Ili uweze Kupakua Nyimbo Mpya kirahisi
> Pia Utapata Taarifa kila wimbo Mpya unapotufikia.

PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file

Official android App for www.cleverwebtz.blogspot.com

This application is developed with the following key features:
• Listening Music online with latest collection of tracks
• Download Music for listening offline
• Read story from different author
•watch movies online and download
• Listen to Music and do other things with a convenient way with playing background modes, customizable through the Notification bar (notification).

PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file

Last Updates

DEREVA TOYO 14