CLEVER WEB TZ

Breaking News
Loading…

Pages

TANGAZA NASI

TANGAZA NASI
ENEZA BIASHARA YAKO

Friday, January 10, 2020

TYPHIN 07


TYPHIN 07
‘Hadithi ya kale, inayoishi’
HUSSEIN O. MOLITO
0718 97 56 59/ 0765 68 4870
“Nataka maji.”
kwa mara ya kwanza aliweza kuisikia sauti ya binti huyo mwenye macho makali ikimuamrisha. Akajikuta akikubali kwa kichwa huku sauti ikigoma kutoka. Akashtushwa na sauti za honi kutoka nyuma yake, maana muda huo taa zilisharuhusu na alikua amebung’aa tu baada ya kumuona binti huyo mwenye maajabu akiwa ndani ya gari yake.
Hakujua alipanda wakati gani, na amemfuata akiwa na nia gani baada ya kumfanyia vitimbi usiku wa siku iliyopita.
Akaondoa gari kwa spidi na kwenda kuiegesha kwenye kituo cha daladala ili aweze kumnunulia maji binti huyo. Akiwa na kitete, alimuita muuza maji na kununua maji yale makubwa kuliko yote kwenye deli lake la kuuzia. Akampatia binti huyo ambaye aliyapokea na kuyatupa nje kwa hasira.
Si inspekta Salim pekee aliyeshangazwa na kitendo hicho, bali hata muuza maji pia alikumbwa na hali hiyo. Ili yasitokee mengine ya kushangaza na kuwafahamisha watu wengine kua hakua na binaadamu wa kawaida ndani ya gari yake, aliamua kuondoa gari na kujaribu kumuhoji binti huyo alikua anahitaji maji ya aina gani.
Ububu ukatawala kwa kila swali alilomuuliza, binti huyo hakujibu kitu chochote zaidi ya kutazama nje na kuduwaa baada ya kuona mazingira yaliyompendeza machoni mwake.
Walipita maeneo ya daraja la Sarenda, ndipo binti huyo alipotabasamu baada ya kuona bahari.
“Simamisha gari.” Binti huyo akatoa amri nyingine, Inspekta Salim hakua na la ziada zaidi ya kuangalia usalama wa eneo hilo na kuegesha gari pembeni.
Kiumbe huyo akashuka na kuelekea upande uliokua na bahari. Hapo ndipo alipomshuhudia akikatisha barabara kila kuangalia magari.
“Kumbe alimaanisha anataka maji ya kuoga!” Inspekta alijisemea baada ya binti huyo kuelekea upande wa baharini. Alitamani kumfuatilia ili aweze kujua ni kipi kilichompelekea atamani kuoga muda huo, ila moyo wenye hofu ukamtuma aendelee na ratiba zake, maana binti huyo anaweza kumdhuru iwapo atagundua kua anamfuatilia. Alihisi kua binti huyo, inawezekana akawa hapendi kuangaliwa sana au kufuatiliwa ndo maana anaamua kuwadhuru wanaadamu au kushambulia magari pindi avukapo barabara.
“Nitaweza kumkamata huyu binti kweli?” Inspekta Salim akajiuliza huku akizidi kumtazama kiumbe huyo anavyoishia kwenye barabara.
Muda huohuo simu yake ikaita. Aliposoma jina, lilitokea la Samira. Akaipokea haraka.
“Inspekta Salim, kuna shida kidogo huku Maabara.” Samira akatanguliza kauli hiyo baada tu ya simu yake kupokelewa.
“kuna kitu gani tena kimetokea?” Inspekta Salim akauliza kwa hamaki.
“Kuna watu wamevamia maabara yetu na kuiba baadhi ya tafiti zetu. Kingine kinachonitia hofu, watafiti wenzangu simu zao bado hazipatikani.”
Taarifa ya Samira ilizidi kumfanya Inspekta Salim azidi kuchanganyikiwa.
“kwa sasa upo wapi?” Inspekta Salim akauliza.
“Nipo Maabara.”
“Nakuja.”
Inspekta Salim akaongea hayo na kukata simu. Hakutaka kumfuatilia tena binti huyo mwenye mauzauza. Lisaa limoja baadae, akafanikiwa kufika maabara na kumkuta Samira akiwa amekaa kinyonge. Muonekano wa maabara hiyo, ulionesha wazi kuvamiwa na kusachiwa.
Akapiga simu kituoni na kuomba msaada. Baada ya muda, walifika askari kadhaa na kuanza uchunguzi wa vitu mbalimbali.
“vipi kuhusu watafiti wenzako, unahisi wanaweza kuwa wamezama huko baharini?” Inspekta akamuuliza Samira baada ya kuhakikisha vitu muhimu vya uchunguzi vikiwa vimechukuliwa na wapelelezi.
“ndo hofu yangu kubwa… maana kulikua na taarifa za kuwepo na kiumbe wa ajabu baharini. Viumbe hao ndo wamewashambulia hawa samaki aina ya Golden, ni nadra sana kuwaona samaki hawa kwakua wanaishi kwenye maji ya kina kirefu na kupendelea kukaa sehemu zenye giza nene. Sasa kushambuliwa kwao ni wazi kuwa kuna viumbe hatari wamesogea baharini.” Samira akatoa maelezo hayo yaliyomfanya Inspekta Salim akune kichwa.
“itabidi niwashirikishe askari wa majini juu ya tukio hili… nadhani watafuatilia na kutupatia majibu sahihi juu ya hili jambo. Kwa sasa ningependa hii maabara ifungwe kwa muda ili kupisha huu upelelezi.” Inspekta Salim akaongea maneno hayo na Samira akakubaliana naye.
*************
Kwenye jengo la sukita, juu kabisa ya ghorofa, Dokta Miley akiwa na vijana wapatao nane waliojazia miili. Walikabidhi baadhi ya vitu kwake na yeye akawakabidhi pesa. Baada ya hapo kila mtu akiondoka kwa njia yake.
Akiwa kwenye gari, Dokta Miley akampigia simu mshirika wake.
“Dokta Maliki, vijana wamefanya kazi nzuri. Nadhani tunaweza kukutana muda huu ili nikukabidhi hii michanganyiko.” Dokta Miley aliongea maneno huyo huku akitabsamu. Akawasha gari yake na kuondoka eneo hilo baada ya kukubaliana ni wapi wawili hao watakutana.
Baada ya Mwendo wa masaa mawili, alifika eneo hilo na kukutana na Dokta Maliki.
“tumebakisha masaa kumi na mbili tu ili tuweze kupata michanganyiko mipya… na hizi tafiti tulizozipata, zinaweza kutusaidia kutengeneza vitu vingine vipya na kupata sifa kwenye serikali hii na Afrika kwa ujumla.” Dokta Maliki akaongea hayo na kumfanya Dokta Miley atafakari jambo.
“hizi tafiti kama zikifanikiwa kutuletea majibu maridhawa, basi inabidi kuna watu wapoteze maisha ili tubaki salama.” Dokta Miley akaongea maneno hayo na kumfanya Dokta Maliki ashtuke.
“wakina nani hao?”
“Mtafiti Gibson na msaidizi wake… maana hao ndo wanasauti kubwa sana serikalini. Wakisema kuwa sisi ndo tumechukua tafiti zao, wataaminika na sisi tutakua hatiani.” Dokta Miley akaongea hayo na kumfanya mwenzake atikise kichwa kama ishara ya kukubaliana naye.
“Mimi nitadili na Mtafiti Gibson, maana mimi ndo mwangalizi wake kule hospitali. Wewe andaa watu wa kuuondoa uhai wa Samira.” Dokta Miley akagawa majukumu na wote wakakubaliana nayo.
Haya, tamaa ya mali na kuwa na majina makubwa kupitia juhudi zilizofanywa na wenzao, zinawafanya Madaktari hawa kuingia katika dhamira ya kufanya mauaji baada ya kuiba tafiti ambazo wanaamini zitakua tiba kwa magonjwa sugu, hivyo zitawasaidia kutengeneza pesa nyingi.
Je Mtafiti Gibson na Samira watauwawa? Kipi kitakachotokea iwapo yatapita masaa 72 bila Inspekta Salim kumkamata kiumbe huyo aliyemshuhudia akielekea baharini?
Ukumbuke tu, hii ni Typhin… wingi wenu kwenye ufuatiliji ndo itakua inakuja mara nyingi kwa wiki.

0 comments:

Post a Comment

comment

PAKUA APP YETU

Kwa wale wapenzi wa Mziki Mzuri,filamu nzuri na Hadithi nzuri kutoka kwa waandishi mbalimbali, blog yetu ya Burudani, Tunapenda Kuwataarifu kuwa:

> Kama Hautumii App Basi tunakuomba PAKUA APP YETU MPYA HAPA Ili uweze Kupakua Nyimbo Mpya kirahisi
> Pia Utapata Taarifa kila wimbo Mpya unapotufikia.

PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file

Official android App for www.cleverwebtz.blogspot.com

This application is developed with the following key features:
• Listening Music online with latest collection of tracks
• Download Music for listening offline
• Read story from different author
•watch movies online and download
• Listen to Music and do other things with a convenient way with playing background modes, customizable through the Notification bar (notification).

PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file

Last Updates

DEREVA TOYO 14