CLEVER WEB TZ

Breaking News
Loading…

Pages

TANGAZA NASI

TANGAZA NASI
ENEZA BIASHARA YAKO

Tuesday, November 26, 2019

Angalia huyu jamaa alivyomuweza huyu binti wa chuo

V.gif Angalia huyu jamaa alivyomuweza huyu binti wa chuo

😁😁😁😁 .. TABU KUDATE NA MADEMU WA CHUO
Demu ; Baby Safari Hii Nataka Pale Hostel Niwafunike Mashoga Zangu Wote.
Jamaa ; Poa Sweetie Ondoa Shaka Nitakununulia #Turubai Utawafunika Wote…!!!
Demu: Mxiuuuuuuuu Lione Sura Kama Goti La mbuzi Na Namba yangu futa Nakublock Mpaka Sanduku la posta…!!! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚nmecheka adi nmelazwa

πŸ˜‚πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚πŸ˜‚

Mambo ya kijijini haya!


Mambo ya kijijini haya!

Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuni…unaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng'ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuni…πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

πŸ˜‚πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚πŸ˜‚

Hadithi za kuchekesha katika Afrika

Hadithi za kuchekesha katika Afrika

Kila wanafunzi katika darasa letu ametembelea Afrika ya mashariki kwa hivyo kila mtu ana hadithi za kuchekesha nafikiri.

Ninaweza kuanza na hadithi moja katika Zimbabwe. Nilienda Zimbabwe kabla ya uchaguzi na niliendesha kati ya Harare na Bulawayo (mji kubwa wa MDC). Kama kawaida pale Afrika, kuna polisi nyingi kando ya barabara na wanazuia kila gari wakati wanafikiri wanaweza kupata pesa au kupata vitu vya upinzani yao. Kwa kivyo nilizuiwa kila wakati niliona polisi kwa sababu mimi si mwafrika na wanajua labda nina pesa na nitalipa. Polisi moja, baada ya kujizuia barabarani, alisema nilihitaji kuwa na leseni ya Zimbabwe kuendesha na itakuwa ada kubwa. Nilisema leseni yangu ilikuwa ya kutosha kuendesha pale na sikuenda kulipa. Halafu alianza kutafuta gari langu wakati nilichungwa na polisi mwengine. Halafu kiongozi cha polisi ambaye alikuwa na bundee kubwa alijaa na alijiona na aliguta, "Wewe ni Peter Crouch!" Nilisema tu, "Mimi si Peter Crouch, jina langu ni Marcus" na alisema "Hapana najua wewe ni Peter Crouch, hamna shida, unaweza kuendelea." Halafu polisi yao walisimama kutafuto na niliondoka bila kulipa.

Baada ya kuondoka Zimbabwe nilijifunza Peter Crouch ni mchezaji maalum wa soka katika Uingereza, na alifanana mimi (labda). Kwa hivyo kiongozi cha polisi alifikiri mimi nilikuwa mchezaji wa soka. Tangu Zimbabwe nimevurugwa na Peter Crouch katika Afrika mara tatu tofauti na kila mara mtu anajiomba kusaini vitu vyao.

BROTHERHOOD (UKAKA) 2


BrotherHood(2)
Mtunzi:Abi
Tulipoishia>>"Baba mzigo ulifika salama ila baadhi ya vijana wetu wamekamatwa na jeshi la polisi"aliongea Jacob.
"Huo ni uzembe mwanangu je wamekamatwa vijana wangapi?" aliongea chris<<
Inaendelea>>"nisamehe baba,wamekamatwa vijana watatu ambao ni Gilbert,Moslin na Timeka"aliongea Jacob kwa upole sana.
"Hahahaha Jacob umekua mpole sana, usijali huo ni mpango wangu"aliongea Chris.
"Unamaanisha nini kusema hivyo baba"aliuliza Jacob akionekana amebaki njia ya panda kwa maneno ya chris.
"Unakumbuka niliwaambia mgawane vikundi na kila kundi lipite njia yao" aliongea Chris kwa njia ya swali kwa lengo la kutaka kumpa maana Jacob.
"Ndio nakumbuka baba"alijibu Jacob kwa shauku ya kutaka kujua maana ya baba yake.
"Unajua mkubwa wa kikundi cha MadDragons ameungana na sisi lakini sio kwa lengo zuri"aliongea Chris.
Jacob akadakia kati kwa kuuliza"una maana gani?"
"usiwe na haraka jacob utaelewa, na wale vijana ni wa kundi hilo kwa niliwachoma kwenye jeshi la polisi ili kummaliza mkubwa wa kundi hilo"aliongea Chris Huku akitabasamu.
**UPANDE WA JUSTIN NA MAMA YAKE**
"Acha kuwaza sana mama,alaf mama unakumbuka kama leo ni siku yako ya kuzaliwa nahitaji tutoke" aliongea Justin akimuangalia mama yake kwa macho ya upendo.
"Ndio wew unanikumbusha sasa hivi"aliongea Jackline.
"Sawa mama basi kajiandae tutoke mimi namalizia kula pia nikajiandae"aliongea Justin.
**UPANDE WA MKUBWA WA KIKUNDI CHA MADDRAGON**
"Bosi nimepokea simu kutoka kwa Chris ,anasema kuwa baadhi ya vijana walikamatwa kwenye ule mpango na walio kamatwa ni vijana wa kundi letu"aliongea Mfuasi wa kundi la Maddragon anayefahamika kwa jina la Stanley.
"Nina wasiwasi huo utakuwa ni mpango wa Chris, na kama ni kweli itakuwa tayari ameshangundua Tulicho kipanga juu yake na kama amejua basi itakuwa kuna msaliti katika kundi letu"aliongea mkubwa wa kundi hilo anafahamika kwa jina la Gerrard.
**KITUO CHA POLISI**
Polisi mmoja alielekea sehemu ya kupiga simu ili kumpa taarifa Justin "Halloo mkuu,hawa wahalifu tumewabana mpaka mmoja wao amekubali kumtaja kiongozi wao".
"Sawa nitafika hapo sasa hivi"aliongea Justin kumjibu polisi huyo kwa njia ya simu.
**UPANDE WA JUSTIN**
"Mama samahani naomba nikurudishe nyumbani nahitaji kwenda kazini"aliongea Justin
"usijali mwanangu"aliongea Jackline .
Kisha wakatoka walipo kuwepo na kuelekea lilipo gari lao.
Wakati wanaelekea kwenye gari Ghafla mlio wa risasi ukasikika "PAaaaaaaaaa" mdogo mdogo Jackline akaanguka chini.
Justin bila ya kupoteza muda akachomoa bastola ndogo na kujibu mashambulizi kisha alim'buruza mama yake kipole pole mpaka kwenye ukuta .
punde si punde vilisikika ving'ora vya gari za polisi.
Kikosi cha maadui kilipo sikia hivyo wakaamua kuondoka eneo hilo.
"vipi uko salama mkuu"aliuliza askari mmoja ambaye ni rafiki pia wa karibu wa Justin anafahamika kwa jina David.
"ndio ,ila nisaidie kuita gari la wagonjwa"aliongea Jacob kumsihi David aite gari la huduma ya kwanza(ambulance).
0623892880/0654445214
ITAENDELEA..........

Sunday, November 24, 2019

BROTHERHOOD (UKAKA)


COPIED PICTURE IF UR THE OWNER CONTACT ME abicleverjunior@gmail.com


Stori: BrotherHood(Ukaka)
Sehemu Ya:1
Mtunzi:Abiclever Yohlo
Mnamo mwaka wa 2000/2/23 majira ya saa 5asubuhi katika bustani ya Nyumba moja ya Tajiri kulikuwa na watoto wawili wa kiume mmoja alifahamika kwa jina la justin na mwengine alifahamika kwa jina la jacob watoto hao walikuwa wakicheza katika mabembea ya nyumba hiyo.
Ghafla ikasikika sauti ya kike ikiwaita, watoto hao waligeuza macho na kuangalia kule iliposikika hiyo sauti.
''Mamii''waliita watoto hao kwa furaha iliyo pitiliza.
kabla watoto hao wajafika kwa mama yao ilisikika sauti nzito "Jackline umefuata nini kwenye nyumba Yangu?" Aliongea Chris Baba wa watoto hao wawili.
"Nimekuja kuwachukua watoto wangu"aliongea Jackline mama wa watoto hao.
"Unataka kuwachukua watoto wangu uwapeleke wapi?"aliongea chris kwa Jazba sana.
"Haikuhusu ujue wapi nawapeleka hawa ni watoto wangu"aliongea Jackline bila ya hofu ya aina yoyote.
"Mlinzi njoo utoe hii taka taka hapa na nisiione tena humu ndani"aliongea chris kumuita mlinzi aje kumtoa jackline.
"Wala usijali naondoka mwenyewe ila nitarudi tena, Kwaherini wanangu nitarudi"aliongea jackline na akaelekea getini.
Jioni ya siku hiyo Chris alipata barua yenye ujumbe kuwa anahitajika mahakamani kesho asubuhi kwa ajili ya kesi ya watoto.
Siku iliyofuata Chris alifika mahakamani,na jackline pia alifika mahakamani.
Saa kazaa zilipita baada ya mahakama kuridhika na maelezo ya pande zote mbili hivyo iliamua kuwa Mama amchukue mtoto mdogo ambaye ni justin na Baba amchukue mtoto mkubwa ambaye ni Jacob.
Japo ilikuwa ngumu kwa pande zote mbili lakini hakukuwa na jinsi hivyo Jackline alienda nyumbani kwa Chris na kumchukua Justin na kwenda kuishi nje kidogo ya mji huo.
*BAADA YA MIAKA 15*
"Mpango huu umeenda sawa kesho tunahitajika kuingia katika mpango mwingine ila na hawa wahalifu tulio wakamata ni lazima tuwabane mpaka waseme ni nani bosi wao" aliongea justin akiwa amevaa mavazi ya Jeshi la polisi na alikuwa ni askari mwenye nyota tatu.
"sawa mkuu"walijibu askari wengine ishara kuwa wamekubaliana na Justin.
Baada ya muda Justin alirejea Nyumbani.
"Mamaaa nimerudi"aliongea Justin Kumjulisha mama yake.
"Sawa mwanangu ila je unajua kama najivunia sana mafanikio yako mwanangu lakini sijui kaka yako anaendelea vipi"aliongea Jackline.
"Baba mzigo ulifika salama ila baadhi ya vijana wetu wamekamatwa na jeshi la polisi"aliongea Jacob.
"Huo ni uzembe mwanangu je wamekamatwa vijana wangapi ?"aliuliza Chris.
0624101615
ITAENDELEA......................

SHABAHA MOJA (ONE TARGET)

                                                            LIKE UKURASA WANGU

Stori : Shabaha Moja(One Target)
Mtunzi: ABiClever Junior
Sehemu: 1
"Jesi ni nini unachowaza mbona umeshika Tama?"aliuliza Ramso kwa shauku ya kutaka kujua anachowaza jeska(jesi).
"Hapana nafikiria sana kuhusu siku yangu ya kuzaliwa ikifika nani atanifariji maana nimebaki yatima kwa sasa" alijibu jesi kwa unyonge sana uku akiendelea kushika tama na chozi likimdondoka jicho la kushoto.
"kweli inauma kutokuwa na wazazi ila mimi nipo jesi na usijali siku hiyo ikifika nina hakika utafurahia uwepo wangu" aliongea Ramso kwa upole ili angalau aweze kutuliza maumivu aliyo nayo Jesi kwa kuwakosa wazazi wake.
"asante ila ata sasa hivi nafurahia uwepo wako Ramso"
"Naapa nipo Tayar kuwa na wewe Bega kwa Bega kuhakikisha Tunalipa kisasi Cha wazazi wako"aliongea Ramso huku akiwa amekutanisha meno yake kwa uchungu.
************MWAKA MMOJA NYUMA*************
ilikuwa ni usiku wa furaha katika Familia ya Bwana Stephano.
"Mwanangu Jeska nakupenda sana na napenda sana kukuona unasoma na kutimiza malengo yako niko tayari kufanya lolote ili mwanangu uweze kuendelea na masomo yako ya Chuo, nimeuza nyumba yangu ile Nyingine ili niweze kupata fedha za kukulipia ada mwanangu" aliongea bwana Stephano.
Ghafla mlio wa Risasi ulisikika mlangoni mwa Nyumba ya Bwana stephano na Mlango ulipigwa teke moja kwa moja watu wanne walio ziba nyuso zao kwa vinyago waliingia ndani na bila ya kuuliza walimpiga Risasi ya ziwa la kushoto Mama Jesi na Kisha walifuata kwa bwana stephano nae pia walimuua kinyama kwa kumchinja shingo. Ving'ora vya Gari za polisi na gari ya kubebea wagonja vilisikika hapo jesi akapata pengo na kuponyoka kwenye mikono ya watu hao.
Baada ya muda kidogo Gari za polisi na Gari la wagonjwa zilifika eneo la Tukio, askari mkuku mkuku walingia ndani kwenye nyumba ya Tukio, askari walitafuta huku na kule hawakuona watu wala mtu zaidi ya zile maiti mbili .
Polisi mmoja aliye fahamika kwa Jina la Ramso alielekea eneo la msalani kwa ajili ya kugagua,huko alikuta mlango umefungwa kwa ndani alipiga teke mlango ule na kumkuta Jesi amejikunyata pembeni kabisa
alimsogelea na Kumuonyesha kitambulisho Jesi ili kumtoa wasi wasi alionao kisha akamshika mkono na Kumtoa Nje kabisa na kisha alimwambia aingie kwenye gari la wagonja, Jesi aliingia ila Baada ya kuingia tu alipoteza Fahamu.
******TUNARUDI MWAKA WA SASA**************
"sawa Ramso wacha mimi niende Chumbani kupumzika kidogo" aliongea Jesi huku akielekea chumbani kwake.
Itaendelea...........................

PAKUA APP YETU

Kwa wale wapenzi wa Mziki Mzuri,filamu nzuri na Hadithi nzuri kutoka kwa waandishi mbalimbali, blog yetu ya Burudani, Tunapenda Kuwataarifu kuwa:

> Kama Hautumii App Basi tunakuomba PAKUA APP YETU MPYA HAPA Ili uweze Kupakua Nyimbo Mpya kirahisi
> Pia Utapata Taarifa kila wimbo Mpya unapotufikia.

PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file

Official android App for www.cleverwebtz.blogspot.com

This application is developed with the following key features:
• Listening Music online with latest collection of tracks
• Download Music for listening offline
• Read story from different author
•watch movies online and download
• Listen to Music and do other things with a convenient way with playing background modes, customizable through the Notification bar (notification).

PAKUA APP YETU MPYA HAPA
BONYEZA HAPA>http://www.mediafire.com/file/qtoi8pn4bj4dqct/Cleverwebtz.apk/file

Last Updates

DEREVA TOYO 14